RITA
JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
Wakala wa Usajili Ufilisi na Udhamini
UDHAMINI
`
Mirathi
FRANK KANYUSI FRANK
Administrator General And Chief Executive Officer

TARATIBU ZA MIRATHI:

  1. Kuteuliwa kwa Kabidhi Wasii Mkuu na Mahakama kama msimamizi wa mirathi, au barua ya mapendekezo toka kwa Katibu Tawala wa eneo ambalo mali zipo kwa usimamizi.
  2. Kabidhi Wasii Mkuu baada ya kuteuliwa na Mahakama au baada ya kupokea barua ya mapendekezo toka kwa Katibu Tawala anatakiwa kupeleka maombi ya usimamizi wa mirathi mahakamani.
  3. Kabidhi Wasii Mkuu baada ya kupewa barua ya usimamizi wa mirathi, anatakiwa kuandaa kikao cha kwanza cha utambulisho na warithi/wanufaika wote wa mirathi husika na kupokea nyaraka za umiliki wa mali zilizopimwa na ambazo hazijapimwa kutoka kwa warithi/wanufaika na taarifa ya usimamizi kutoka kwa msimamizi wa awali kama alikuwepo.
  4. Warithi/wanufaika kupewa fomu A.G.7 wakajaze kwenye ofisi ya Katibu Tawala ambaye marehemu alipokua anaishi au kufariki.
  5. Maelezo ya fomu A.G 7 yanajumuisha maelezo binafsi, maelezo ya warithi/wanufaika, maelezo ya mali za marehemu na madeni kama yapo.
  6. Kabidhi Wasii Mkuu atafanya upekuzi maalumu wa historia ya umiliki wa mali za marehemu kwaajili ya kuhakiki.
  7. Utambuzi na ukaguzi wa mali za marehemu zinazohamishika na zisizohamishika.
  8. Kabidhi Wasii Mkuu atafanya taratibu za kuhamisha mali zilizopimwa (ardhi) toka kwenye jina la marehemu kwenda kwenye jina lake kwaajili ya usimamizi.
  9. Kufanya tathimini ya mali zilizotambuliwa na kuandaa kikao kuwajulisha warithi/ wanufaika kuhusu maendeleo ya usimamizi wa mirathi ya marehemu. Kikao hiki kitahusisha uhakiki wa madeni  ya marehemu  ikiwajumuisha warithi.
  10. Kuwasilisha orodha ya mali mahakamani.
  11. Kulipa madeni ya marehemu.
  12. Mgawanyo wa mali kwa warithi/wanufaika halali, kulipa madeni, ada ya usimamizi na gharama pamoja na kodi za Serikali zilizojitokeza.
  13. Kuwasilisha mahesabu ya mwisho Mahakamani.
  14. Kuhamisha umiliki wa mali toka kwenye jina la Kabidhi Wasii Mkuu kwenda kwa warithi/wanufaika halali.
  15. Kufungwa kwa mirathi na Kabidhi Wasii Mkuu kuondolewa kwenye usimamizi.

1: USIMAMIZI WA MIRATHI

  • Kuteuliwa kwa Kabidhi Wasii Mkuu na Mahakama kama msimamizi wa mirathi, au barua ya mapendekezo toka kwa Katibu Tawala wa eneo ambalo mali zipo kwa usimamizi.
  • ·       Kabidhi Wasii Mkuu baada ya kuteuliwa na Mahakama au baada ya kupokea barua ya mapendekezo toka kwa Katibu Tawala anatakiwa kupeleka maombi ya usimamizi wa mirathi mahakamani.

    ·       Kabidhi Wasii Mkuu baada ya kupewa barua ya usimamizi wa mirathi, anatakiwa kuandaa kikao cha kwanza cha utambulisho na warithi/wanufaika wote wa mirathi husika na kupokea nyaraka za umiliki wa mali zilizopimwa na ambazo hazijapimwa kutoka kwa warithi/wanufaika na taarifa ya usimamizi kutoka kwa msimamizi wa awali kama alikuwepo.

    ·       Warithi/wanufaika kupewa fomu A.G.7 wakajaze kwenye ofisi ya Katibu Tawala ambaye marehemu alipokua anaishi au kufariki.


    ·       Maelezo ya fomu A.G 7 yanajumuisha maelezo binafsi, maelezo ya warithi/wanufaika, maelezo ya mali za marehemu na madeni kama yapo.


    ·      Kabidhi Wasii Mkuu atafanya upekuzi maalumu wa historia ya umiliki wa mali za marehemu kwaajili ya kuhakiki.


    Utambuzi na ukaguzi wa mali za marehemu zinazohamishika na zisizohamishika.

    ·       Kabidhi Wasii Mkuu atafanya taratibu za kuhamisha mali zilizopimwa (ardhi) toka kwenye jina la marehemu kwenda kwenye jina lake kwaajili ya usimamizi.


    ·       Kufanya tathimini ya mali zilizotambuliwa na kuandaa kikao kuwajulisha warithi/ wanufaika kuhusu maendeleo ya usimamizi wa mirathi ya marehemu. Kikao hiki kitahusisha uhakiki wa madeni  ya marehemu  ikiwajumuisha warithi.


    ·      Kuwasilisha orodha ya mali mahakamani.


    ·       Kulipa madeni ya marehemu.


    ·       Mgawanyo wa mali kwa warithi/wanufaika halali, kulipa madeni, ada ya usimamizi na gharama pamoja na kodi za Serikali zilizojitokeza.


    ·       Kuwasilisha mahesabu ya mwisho Mahakamani.


    ·       Kuhamisha umiliki wa mali toka kwenye jina la Kabidhi Wasii Mkuu kwenda kwa warithi/wanufaika halali.


    ·       Kufungwa kwa mirathi na Kabidhi Wasii Mkuu kuondolewa kwenye usimamizi.

Ona Ukurasa Kamili
Washirika wetu
Wadau Wetu